Pages

Ads 468x60px

Tuesday, April 7, 2015

WANANCHI WATAKIWA KUWEKA MAZINGIRA YAO SAFI




Wananchi wametakiwa kuwa na tabia ya kuweka mazingira yao katika hali ya usafi kwani ni swala  muhimu katika maisha ya mwanandamu.

 Wito huo umetolewana AYASY RAMADHAN operation manager wa kampuni  ya
Ayasy Ramadhani Operation manager
ASAKYS INVESTMENT inayoshughurika na usafi Mkoani Mbeya.
Amesema hayo katika zoezi la uondoaji taka katika ghuba lililopo katika kata ya Sisimba ambalo halijatolewa taka zaidi ya miezi sita na kusababisha usumbufu kwa wakazi aeneo hilo kwa harufu mbaya na kutaka kuwahatalishia afya zao magonjwa ya milipuko.

“leo tupo katika eneo hili la kata ya Sisima kwajili ya zoezi la kuweka mji wetu katika hali ya usafi natoa wito kwa wakazi wa kata hii kutunza mazingira na kuyaweka katika hali ya nzuri, kwani inawezekana kuishi bila uchafu tuige mikoa  mingine wameweza kutunza mazingira yao” amesema Ayasy

Ameongeza kuwa swala hilo niendelevu kwa sasa wapo katika hatuo ya mwanzo katika kuziondoa taka baada ya hapo wataweka vyombo maarumu vya kuhifadhia.
 Aidha ametoa angalizo kwa mtu yoyote atakae kutwa akitupa taka hovyo atakamatwa na kulipa faini isiyopungua Tshs 50,000/=

Kwa upande wake JOFREY KAJIGILI diwani wa kata ya hiyo amewataka wananchi wa kata yake kutoa ushirikiano na kampuni ya ASAKYS INVESTMENT  katika kufuata ratiba ya kuondoshwa taka katika mitaa yao ili iwe rahisi kufanya kazi na kata yake iwe ya mfano wa kuigwa na kata zingine, akitolea mfano mji wa moshi.

ASAKYS INVESTMENT ni kampuni yenye makao yake mkuu jijini Mbeya inayo jishughulisha na mambo ya usafi na kwa sasa imechukua tenda ya uondoswaji wa  taka katika kata mbili ikiwepo ile ya forest.

                                                   Mwisho 
                                  Ayasi akiongea na waandishi wa habari
                              Jofrey kajigili diwani wa kata ya sisimba





 Meneja na diwani wa kata ya sisimba wakionesha mfano katika kuwajibika kutekeleza swala la usafi





                           Gari la taka likipita katika kata ya Forest kukusanya taka

0 comments:

Post a Comment