Pages

Ads 468x60px

Monday, April 13, 2015

WATANZANIA WASHAULIWA KUISOMA VIZURI KATIBA NA KUIPIGIA KURA YA NDIYO



Watanzania wametakiwa kuipitia katiba pendekezwa  kwa makini kisha kuamua  kuipigia kula ya ndiyo au hapana.
 Haya yamebainishwa na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Abdallah bulembo wakati  akifungua shina la wazazi  katika kata ya  majengo jijini  Mbeya

Abdallah Bulembo
Bulembo amesema wananchi  wasisikilize  watu katika kutoa  mawazo yao ya nini k katika ifanyike katiba kwani kila mmoja anawajibu wakujua nini anapaswa kukifanya juu ya katiba pendekezwa

Amesema katiba  inayopendekezwa   ni kwa mustakabali  wa kizazi kijacho na wanatakiwa kujua kuwa maamuzi yoyote mabaya yatakayo amuliwa ni mateso kwa watoto wakizazi hicho.



“Ndugu zangu ichukueni katiba pendekezwa isomeni vizuri na kuipigia kura ya ndiyo au hapana hii ni kwa ajili ya watoto wenu nyie ya kwenu imeshapita miaka hamsini iliyopita  na miaka mingine ambayo sisi tutakua tumekufa hivyo tusiamue kitu mabacho tutalaumiwa na vizazi vijavyo. Acheni ushabiki katika kuamua kitu muhimu kama hiki” amesema Bulembo

Shina la wazazi lazinduliwa majengo
Ameongeza kuwa katiba hii ikipita itaanza kufanya kazi mwaka 2020  kwani kwa sasa bado katiba iliyopo itaendelea kufanya  kazi  inaendelea kufanyiwa  mchakato wa kuitengeneza, endapo itapigiwa kura ya hapana  itaendelea kutumika ile ya zamani.

Pia amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwenye  daftari la kudumu  la wapigakura na  uchaguzi wa viongozi unaotarajia kufanyika mwaka huu .







                                                                          Mwisho


 Abdallah Bulembo akiwasili katika kata ya majengo na kusalimiana na viongozi wa kata hiyo

Katibu  wa wilaya ya Mbeya mjini akiongea na wakazi wa kata ya majengo baada ya kuwasili katia soko la majengo.

                                                            Watoto hawakua nyuma












Bulembo awaongoza shangwe mamia ya wanachama wa (CCM) walojitokeza kumsikiliza katika soko la majengo kabla ya kuwahutubia




 Viongozi mbalimbali walio ongozana na Bulembo wakiongozwa na mwenyekiti wa wazazi mkoa wa mbeya Fatuma Kassenga

Andrew Msaso mwenyekiti wa wazazi kata ya majengo akiongea kitu kwa mgeni rasmi

                Islam Rajabu katibu wa wazazi mkoa wa mbeya akisoma risala mbele ya mgeni rasmi
 Bulembo akihutubia wananchi waliojitokeza katika uzinduzi wa shina la wazazi katika kata ya majengo.





                                                           Bulembo akizindua shina la Regco


                                Bulembo akizindua kituo cha waendesha boadaboda wa majengo
                        Viongozi na wazee wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi


0 comments:

Post a Comment