Pages

Ads 468x60px

Tuesday, April 14, 2015

WATANZANIA WASHAURIWA KUIKATAA KATIBA PENDEKEZWA KUTOKANA NA KUKIUKA MAONI YAO




Wakati  harakati za mashirika yasiyo ya Serikali yakiendelea kutoa elimu juu ya katiba pendekezwa kablaya kupigiwa kura na kuwa katiba kamili, Mkurugenzi mtandaji wa Taasisi ya mwalimu Nyerere JOSEPH BUTIKU amewataka wananchi kuipigia kura ya hapana katiba pendekezwa.

Joseph Butiku
Ameyasema hayo katika mdahalo uliofanyika katika ukumbi wa chuo kikuu (TEKU) wakati  wakitoa maoni yaliyotolewa katika tume ya waryoba kwamba katiba hiyo haijazingatia kile kilichomo katika rasmu hiyo.
elimu ya uraia na kulinganisha

“Isomeni katiba vizuri na kuipigia kura ya hapana kwani mkifanya hivyo italazimu kuipitia upya kutokana na kwamba katiba pendekezwa imeondolewa maono yenu mengi  ikiwepo mamlaka ya Raisi, mbunge kuwajibishwa na wapiga kura wake, mawaziri wasitokane na wabunge nk” wamefanya hivyo kutaka kutetea maslahi yao na kuwakandamiza wananchi” amesema hayo Butiku

Na HANCE POLEPOLE amesema katiba ni mkataba kati ya wananchi na viongozi wanao waongoza na hviyo wanatakiwa kuwa makini katika kutengeza mkataba  ili wasije laumiwa na vizazi vijavyo kwa kushindwa kutengeneza katibayenye maslahi  yao  na kuwafanya wengine watumwa katika nchi yao kwani  kila mtu ana haki ya kufaidi kwa usawa. 

                                                                           Mwisho 
Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya mwalimu Nyerere akifungua madahalo katika ukumbi wa chuo kikuu (TEKU)
             Hance polepole mmoja wa watoa mada akizungumzia kitu katika katiba pendekezwa
                                                      Ally Sarehe mmoja wa watoa mada 
                                                Pof: Mwesigwa Balegu mmoja wa watoa mada





          Baadhi ya watu waliojitokeza kusikiliza mdahalo katika ukumbi wa chuo kikuu (TEKU)



                     Baadhi ya watu walipata fursa ya kuuliza maswali katika mdahalo huo

                            Kakulu mwandishi wa habari wa kituo cha Habari cha Azam Tv

0 comments:

Post a Comment