·
Ni hifadhi inayopatikana katika Wilaya ya Rungwe Mkoa wa
Mbeya. Ilihifadhiwa Mwaka 1949 kwa lengo la kuhifadhi vyanzo vya maji na
baionuai (biodiversity). Ukubwa wake ni hekta 13,652.1. Hifadhi hii ipo umbali
wa km 25 kusini Mashariki mwa mji wa Mbeya na umbali wa km 7 kaskazini mwa mji
wa Tukuyu
Kipunji Nyani adimu duniani |
·
Hifadhi Asilia ya Mlima Rungwe inamilikiwa na serikali kuu
chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Usimamizi wake uko chini ya Wakala wa
Huduma za Misitu Tanzania (TFS). Wakala huu ulianzishwa mwaka 2010 kwa ajili ya
kusimamia rasilimali za misitu na nyuki kwa tangazo la serikali na. 269 la
tarehe 30/07/2010
·
Baada ya kuona umuhimu mkubwa wa hifadhi ya Mlima Rungwe,
mchakato wa kupandisha hadhi ulianzishwa mwaka 2008 na hatimaye mwaka 2009
hifadhi ilipandishwa hadhi na kuwa Hifadhi ya Mazingira Asilia. Hifadhi ya
Mazingira Asilia ni hadhi ya juu kuliko Msitu wa Hifadhi. Hifadhi ya Mazingira
Asilia hairuhusu matumizi mengine zaidi ya elimu, utafiti na utalii.
·
Katika kusimamia Hifadhi ya Mazingira Asilia, msimamizi ni
Mhifadhi Mkuu (Conservator)
ambaye huripoti kwa Meneja wa Kanda. Mhifadhi Mkuu
anasaidiwa na Maafisa Misitu ambao wako katika vituo vya Syukula, Kandete,
Tukuyu na Unyamwanga.
Kipunji stealing maize cobs |
·
Kwa Tanzania, kuna hifadhi 11 tu zenye hadhi ya Mazingira
Asilia ambazo ni Mlima Rungwe, Kilombero (Iringa), Uzungwa (Iringa), Uluguru
(Morogoro), Mkingu (Morogoro), Rondo (Lindi), Amani (Tanga), Chome
(Kilimanjaro), Nilo (Tanga), Minziro (Kagera) na Magamba (Tanga).
·
Hifadhi ya Mlima Rungwe imezungukwa na Vijiji 23 kama
inavyooneshwa hapa chini. Hatahivyo vijiji vinavyogusa hifadhi moja kwa moja ni
16 tu.
Vijiji vinavyozunguka Hifadhi Asilia Mlima Rungwe
Kijiji
|
Kata
|
Tarafa
|
Idadi ya watu
(sensa ya 2002)
|
Idadi ya watu ( sensa ya 2012)
|
Mabadiliko %
|
|
1
|
Bujingijila
|
Kandate
|
Busokelo
|
828
|
872
|
5
|
2
|
Ndala
|
Kandate
|
Busokelo
|
2 541
|
1 777
|
-43
|
3
|
Lugombo
|
Kandete
|
Busokelo
|
934
|
781
|
-20
|
4
|
Katumba
|
Katumba
|
Pakati
|
5 255
|
6 452
|
19
|
5
|
Ibumba
|
Suma
|
Pakati
|
1 165
|
1 136
|
-3
|
6
|
Masebe
|
Katumba
|
Pakati
|
1 255
|
1 375
|
9
|
7
|
Kabale
|
Suma
|
Pakati
|
998
|
909
|
-10
|
8
|
Ngumbulu
|
Isongole
|
Ukukwe
|
115
|
1 107
|
90
|
9
|
Ilundo
|
Kiwira
|
Ukukwe
|
4 051
|
4 694
|
14
|
10
|
Nditu
|
Suma
|
Ukukwe
|
2 391
|
2 415
|
1
|
11
|
Syukula
|
Kyimo
|
Ukukwe
|
4 653
|
4 461
|
-4
|
12
|
Ikama
|
Katumba
|
Ukukwe
|
1 682
|
1 415
|
-5
|
13
|
Ndwati
|
Isongole
|
Ukukwe
|
431
|
392
|
-10
|
14
|
Mpandapanda
|
Kiwira
|
Ukukwe
|
6 308
|
8 356
|
25
|
15
|
Isyonje
|
Isongole
|
Ukukwe
|
1 631
|
1 389
|
-17
|
16
|
Ndaga
|
Isongole
|
Ukukwe
|
4 044
|
5 056
|
20
|
17
|
Mbeye one
|
Isongole
|
Ukukwe
|
961
|
1 167
|
18
|
18
|
Kibisi
|
Kyimo
|
Ukukwe
|
1 728
|
1 678
|
-3
|
19
|
Ilolo
|
Kiwira
|
Ukukwe
|
3 891
|
3 239
|
-20
|
20
|
Unyamwanga
|
Isongole
|
Ukukwe
|
1 502
|
1 372
|
-9
|
21
|
Ntokela
|
Isongole
|
Ukukwe
|
3 390
|
6 438
|
47
|
22
|
Idweli
|
Isongole
|
Ukukwe
|
1 864
|
1 768
|
-5
|
23
|
Suma
|
Suma
|
Ukukwe
|
976
|
839
|
-16
|
Jumla
|
52, 594
|
59 ,091
|
|
Umuhimu wa Hifadhi
ya Mazingira Asilia Mlima Rungwe
- Chanzo cha maji (mito inayo tiririka kutoka kwenye hifadhi)
Mito hii ina
umuhimu mkubwa kwa vijiji na miji kadhaa kama Katumba, Kiwira, Kandete na
sehemu zingine. Mito hii ni kama; siniki, marogala, kipoki, kilasi, Mulagala na
mingineyo ambayo maji yake yanaingia Ziwa Nyasa. Imefahamika kuwa mito hii
huchangia asilimia 48 ya maji ya ziwa Nyasa. Aidha kilimo katika bonde la ziwa
Nyasa hutegemea sana maji kutoka hifadhi hii
2.
Kurekebisha Hali ya hewa
Uwepo wa hifadhi
hii umepelekea kuwa na hali ya hewa safi ndani ya wilaya ya Rungwe na maeneo
mengine ambayo imechujwa na mimea, pia inachangia kuvuta mvua za kutosha kama
matokeo ya uhifadhi wa mazingira ukilinganisha na sehemu zingine ambako kuna
uhaba wa misitu na kama ipo haitunzwi ipasavyo
3.
Uchumi kutokana na
Utalii
Kutokana na sifa za kipekee za Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Mlima Rungwe: ikiwemo
urefu wa mlima, mashimo ya volukano (paluvalutali, Lusiba na Ng’ombe) na
wanyama aina ya kipunji, na maji moto. Vyote hivi vimekuwa vinashawishi watalii
kutembelea hifadhi yetu ya mazingira asilia ya mlima Rungwe. Pia hifadhi
imepakana na hifadhi ya Kitulo ambayo ina vivutio vingi vya kitalii
4.
Hifadhi ya baionuai muhimu
5.
Huchangia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na mabadiliko ya
tabianchi
Kazi zinazofanyika
katika kuhifadhi
Katika kuhakikisha kuwa hiafadhi hii inabakia kuwa katika hali ya
kuridhisha, shughuli mbalimbali hufanyika ikiwa ni pamoja na;
i.
Kusafisha mipaka, kazi hii inafanyika kila mwaka wakati wa
kiangazi. Hii inasaidia kuzuia uvamizi hasa unaotokana na shughuli za kilimo
ii.
Doria za mara kwa mara. Kazi hii hufanyika kwa kushirikisha
kamati za Mazingira za Vijiji, skauti na vyombo vya usalama
iii.
Utoaji wa elimu. Lengo la kazi hii ni kuongeza uelewa kwa
jamii inayozunguka hifadhi ili iendelee kushiriki kikamilifu katika kuhifadhi
mazingira.
iv.
Uwekaji wa alama za kudumu kwenye mipaka na njia za
kuingilia kwenye hifadhi. Alama hizi ni pamoja na maboya (beacons), mabango na
mahandaki ya uelekeo (directional trenches)
v.
Uanzishaji wa vitalu vya miche ya miti kwa ajili ya jamii
inayozunguka hifadhi
Mapato kutoka katika hifadhi Mazingira Asilia Mlima
Rungwe
Kama ilivyoelezwa
awali kuwa hifadhi hii ni kwa ajili ya mafunzo, utafiti, na utalii ikolojia tu.
Hakuna uvunaji wowote ule unaofanyika. Kwahiyo hifadhi hii inapata mapato
kutokana na ada za utafiti na za utalii tu. Kwa mfano katika kipindi cha
Februari 2014 hadi Juni 2015 utalii uliingiza kiasi cha TSH 6,007,655/- kiasi
ambacho ni asilimia 0.7 ya bajeti ya kusimamia hifadhi kwa mwaka mmoja. Asilimia 5 ya
makusanyo hupelekwa Halmashauri kwa mujibu wa sheria. Kiasi hiki kinapaswa
kupelekwa katika vijiji kupitia halmashauri kwa ajili ya kutekeleza shughuli
mbalimbali za kimaendeleo.
Changamoto katika utekelezaji wa shughuli za kuhifadhi
Hifadhi yetu hii inakabiliwa na changamoto zifuatazo:
i.
Ufinyu wa bajeti kwa ajili
ya kufanikisha uhifadhi; mfano: kufanya doria za kina na tahadhari ya moto, na
tafiti mbalimbali.
ii.
Upungufu wa vitendea kazi;
mfano magari na rasilimali watumishi.
iii.
Miundo mbinu ya barabara na
majengo kwa ajili ya ofisi na watu
iv.
Miti vamizi (pine)
v.
Uvunaji haramu wa mbao,
mkaa, na mazao mengine ya misitu. Aidha uwindaji haramu wa wanyama kama Kipunji
na Minde unafanywa na baadhi ya wanakijiji wasio waaminifu.
vi.
Moto kutoka kwenye mashamba
ya watu, wawindaji na urinaji asali usio fuata utaalam wa kisasa
vii.
Ushiriki usioridhisha kutoka kwa baadhi ya vijiji
vinavyozunguka hifadhi. Baadhi ya vijiji vimekuwa vikikataa kushiriki katika
kuhiafadhi hasa shughuli kama za kuzima moto. Hii inatokana na madai kwamba
hawaoni faida zinazotokana na hifadhi hii.
Hali Halisi ya Hifadhi ya Mlima Rungwe
Hifadhi
Asilia ya Mlima Rungwe imeboreka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na kipindi
cha miaka 5 iliyopita. Matukio mengi ya uharibifu kwa kukata miti na kilimo
yamepungua kwa kiasi kikubwa.
·
Kwa sasa hifadhi hii ina tatizo la uvamizi wa miti ya
kigeni (Pinus patula). Miti hii
iliripotiwa na WCS kwa mara ya kwanza mwaka 2004 ikiwa imevamia hekta 64. Hadi
sasa eneo ililovamiwa ni zaidi ya hekta 100.
·
Matukio ya moto. Hili ni tatizo kubwa ambalo huathiri
hifadhi kwa kiasi kikubwa sana. Uoto wa asili na wanyama hasa wado wadogo
hupotea. Mwaka 2009 moto uliteketeza takribani hekta 2,000 za uoto hasa ukanda
wa nyasi (grasslands). Mwaka 2015 moto uliteketeza takribani hekta 1,200 ambao
pia uliteketeza eneo la nyasi. Vyanzo vya moto katika hifadhi ya Mazingira
Asilia Mlima Rungwe ni uwindaji na kilimo.
Upekee wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Mlima Rungwe
·
Hifadhi Asilia ya Mlima Rungwe ni ya kipekee kwa kuwa na
uoto aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na msitu wa mlimani (lower and upper
montane forests), ukanda wa mianzi (bamboo belt), heathland, mchanganyiko wa
miti mifupi na nyasi (woodland), na nyasi (grassland).
·
Ni sehemu ambayo sampuli ya nyani apatikanaye Tanzania
pekee (Rungwecebus kipunji) ilichukuliwa
na hivyo nyani kupewa jina la Rungwe kwa ukumbusho huo
·
Volkano iliyotulia yenye mashimo ya kuvutia (volcanic
craters)
·
Ni Mlima wa tatu kwa urefu Tanzania ukiwa na urefu wa meta
2,981 baada ya Kilimanjaro (5595m) na Meru (4,600m).
·
Makazi ya vinyonga wenye pembe tatu wapatikanao katika
hifadhi hii pekee
Washirika katika kuhifadhi Msitu Mazingira
Asilia Mlima Rungwe
Hifadhi
Asilia ya Mlima Rungwe inapata michango ya kihifadhi kutoka kwa wadau
mbalimbali kama vile;
1. Shirika la
Kuhifadhi Wanyamapori na Mazingira (Wildlife Conservation Society). Shirika
hili limekuwa likifanya kazi mbalimbali za kuhifadhi Mlima Rungwe tangu miaka
ya 2003. Shiriki hili hufanya kazi mbalimbali hasa za utafiti, utoaji elimu kwa
jamii na kusaidia miradi mbalimbali ya kuongeza kipato kwa jamii inayozunguka
hifadhi. Shughuli hizo ni pamoja na miradi ya ufugaji nyuki, upandaji miti n.k
2. SPANEST
(Strengthening Protected Areas Network for Southern Tanzania).
3. HIMARU (Hifadhi
Mazingira Rungwe)
4. African Wildlife
Foundation (AWF). Shirika hili kwa sasa linasaidia kutengeneza mpango wa
Usimamizi (Management Plan) wa Hifadhi hii.
5. Jamii
zinazozunguka hifadhi
6. Halmashauri ya
Wilaya Rungwe
7. GEF/UNDP. Haya ni
mashirika ya kimataifa ambayo kwa sasa yametoa ufadhili kupitia mradi unaoitwa
“Enhancing Forest Nature Reserves Network for Biodiversity Conservation in
Tanzania”. Mradi huu utafadhili shughuli mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa ofisi,
utengenezaji wa barabara, njia za kitalii, ununuaji wa vitendea kazi mf. Magari
na pikipiki; uwekaji wa mabango n.k.
Mikakati ya baadaye ili kuboresha hifadhi
Hifadhi
ya Mazingira Asilia Mlima Rungwe ina mikakati mbalimbali ili kuboresha uhifadhi
wa Msitu wa Hifadhi Mazingira Asilia Mlima Rungwe
1. Kuboresha
miundombinu ya barabara na njia za utalii
2. Kuingia
makubaliano (Joint Management Agreements) na jamii inayozunguka hifadhi ili wajue
kwa kina faida za hifadhi hii na baadaye washiriki vizuri zaidi katika
kuhifadhi Mlima Rungwe
3. Kutangaza hifadhi
kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni pamoja na websites, blogs
4. Kupandisha hadhi
kutoka Hifadhi Mazingira Asilia na kuwa Urithi wa Dunia (world Heritage)
Mpango wa kuondoa miti vamizi
Hifadhi
hii tayari ina mpango wa usimamizi ambao utaanza kutekelezwa mwaka huu 2016.
Katika mpango huu, kuna mpango mdogo wa kuondoa miti vamizi aina ya misindano
(Pines) kama ilivyoainishwa awali. Miti ya misindano ni tatizo kubwa katika
hifadhi ya Mlima Rungwe kwani inahatarisha ikolojia yake. Tatizo la miti vamizi
halipo katika hifadhi hii tu bali katika maeneo mengine kama vile Hifadhi ya Taifa
ya Kitulo.
Katika kutekeleza
mpango mdogo wa kuondoa miti vamizi, hatua kadhaa tayari zimefikiwa ikiwa ni
pamoja na kuwasilisha andiko (proposal) makao makuu TFS. Katika mpango huo
mdogo tunataraji kufuata hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kupima ujazo wa miti
na eneo lililovamiwa kasha kutoa elimu kwa jamii inayozunguka hifadhi juu ya
kusudio la kuiondoa miti hiyo. Hii itahusisha pia viongozi mbalimbali katika
ngazi za kata na wilaya. Shirika la WCS litasaidia katika kufanikisha zoezi
hili. Aidha uondoaji wa miti hii unatarajiwa kufaidisha TFS na jamii
inayozunguka hifadhi.
0 comments:
Post a Comment