Pages

Ads 468x60px

Thursday, February 4, 2016

Mawakili wa kujitegemea ndio chazo cha kesi kuchelewa kuisha mahakamani



Wakosolewa kua wabinafsi wa kukumbatia kesi nyingi,


Wakili wa serikali mkuu Joseph Pande

Katika maadhimisho ya kilele cha wiki ya Sheria nchini, mawakili wa kujitegemea wakosolewa wameonekana ndio chanzo cha kuchelewesha mwenendo wa kesi mahakamani kwakua wamekua na ubinafsi na kulundikana na kesi nyingi na hivyo kushindwa kumudu na kusababishe kesi kuchelewa kuisha kwa wakati.

Hayo yamebainishwa na wakili wa serikali mkuu mfawidhi wa ofisi ya mwana sheria mkuu JOSEPH PANDE alipokua akitoa taarifa ya mwenendo wa kesi kwa mwaka ulio pita 2015 katika kilele cha sherehe za wiki ya sheria zilizo fanyika katika ukumbi wa mkapa jijini Mbeya

PANDE amesema kumekuwepo na sababu nyingi zinazo sababisha kesi kuchelewa kuisha kwa wakati katika mahakama zetu ikiwa ni pamoja na mawakili hao kukumbatia kesi nyingi kwa wakati mmoja na kusababisha hakimu kuahilisha kila wakati kusikiliza kesi kutokana na mawakili wa kujitegemea kushindwa kumudu muda kwa sababu ya mlundikano wa kesi zao.

“Mahakama imejitahidi kumaliza kesi zote zilizo fika mahakamani hapo kusikilizwa, Kesi zilizo baki ni zile zinazo endeshwa na  mawakili wa kujitegemea wamekua wabinafsi sana katika kazi zao hawataki kugawana ili waweze kumudu na kuzimaliza kwa muda muafaka, Ninawashauri waanzishe makampuni ambayo yatakua na mawakili wengi hivyo kumudu kesi zote kwa muda muafaka” amesema PANDE

Ameongeza kua sababu zingine zinazo sababisha ucheleweshwaji wa kesi mahakamani ni pamoja na vyombo vya upelelezi kushindwa kuharakisha upelelezi kwa wakati, mambo mengine  ni pamoja na waendesha mashitaka kutojipanga kuleta mashahidi  mahakamani kwa muda muafaka na mambo mengine mengi.

Nae Jaji mfawidhi kanda ya Mbeya NOELI CHOCHA amempongeza raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania wa awamu ya tano JOHN POMBE MAGUFURI kwa juhudi zake za wazi kwa huduma za serikali yake zenye kusudi la kumlenga mwananchi moja kwa moja katika kuletea maendeleo sana wale wa kipato cha chini.

“Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza raisi kwa juhudi zake za wazi kwa huduma za serikali yake kumlenga mwananchi moja kwa moja kwakua serikali bila mwananchi ni uhaini na udikteta hivyo huduma za serikali kumlenga mwananchi ni haki kwakua ndiyo waliyo iweka madarakani” amesema CHOCHA.

Kwa upoande wake mgeni wa heshima wa sherehe hizo mkuu wa mkoa wa Mbeya  ABBAS KANDORO amewapongeza watumishi wa mahakama kwa jinsi walivyo anziaha mahakama ktika mji wa chapwa wilayani momba na amewataka waanzishe mahakama nyingine mkwajuni wiy a ya chunya mkoani mbeya.
                         Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas kandoro akiongea na wadau wa sheria
 Jaji mfawidhi kanda ya Mbeya akikagua gwalide kabla ya kuelekea katika ukumbi wa mkapa kwa ajili ya sherehe.





Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro aliepo katikati ya majaji akiongoza maandamano kuelekea ukumbi wa mkapa.



 Baadhi ya mahakimu na mawakili wa serikali na wa kujitegemea walio shiriki maadhimisho ya sherehehe
                                                    Viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama

                                                                        Viongozi wa dini

                                                             Watumishi wa mahakama na polisi

                         Kwaya ya mahakama ikitumbuiza katika sherehe za siku ya sheria nchini

 

0 comments:

Post a Comment