Pages

Ads 468x60px

Friday, February 12, 2016

MJASILIA MALI AOMBA UFADHILI WA MASHINE YA KUKAMUA MAFUTA YA MAWESE



MJASILIA MALI JOTHAM MWANDIBWA AKIZUNGUSHA MASHINE YAKE KUKAMUA MIWESE

Katika hali ya kukabilia na naisha kijana aliejulikana kwa jina la Jotham Mwandibwa ameziomba asasi na mashirika mbalimbali yenye uwezo wa kumkopesha mashine ya kukamua mafuta ya mawese ya kisasa, ili kuboresha biashara yake hiyo ili aweze kumudu kutunza famila yake.

Mwandibwa ameyasema hayo alipotembelewa na mwandishi wa Blog hii kiwandani kwake ambako anendesha shughuli za ukamuaji  wa mafuta  hayo kwa mashine ya kienyeji, iliyo jengwa kwa pipa la bati ndani yake kukiwa na vipande vya nondo vinavyowezesha kusaga na kubangua mbegu za muwese na kupatikana kwa mafuta ya kupikia na sabuni za kufulia   .

“Ninaomba Tasisi au shirika lolote linaloweza kuniwezesha kupata mashine ya kisasa itakayoweza nisaidia kuboresha mradi wangu huu wa kukamua mafuta ya mawese ili niweze kumudu kupambana na maisha kwani biashara yangu inawateja wengi lakini mashine hii duni nashindwa kumudu soko, nikipata mtu wa kunikopesha mashine ya kisasa itaniwezesha kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi” amesema mwandibwa.

Mwandibwa mwenye familia ya mke na watoto sita ambao ni mapacha matatu anae ishi kijiji cha Lwifwa kata ya kisiba wilaya ya Rungwe Mkoani mbeya amekua akitegemea biashara yake hiyo  kuendesha na kutunza familia yake.

                HATUA YA KWANZA NI KUCHEMSHA KABLA YA KUKAMUA MAFUTA
ROBERT SOKAPO AKIMSAIDI BABA YAKE KUFANYA USAFI ENEO LA KUKAMULIA MAFUTA

                                       SHUGHURI YA UKAMUAJI INAENDELEA

BAADA YA KUKAMULIWA MAFUTA HAYO HUJAZWA KATIKA PIPA NA KISHA KUENGU YALIYOIBUKA JUU KAMA UNAVYO MUONA MAJASILA MALI HUYU

 BAADA YA KUENGULIWA HURUDISHWA TENA KATIKA MOTO ILI KUPATA MAFUTA HALISI
BAADA YA MUDA HUIPULUWA NA TAYALI MAFUTA YA MAWESE YAMEPATIKANA
                                              BAADA YA KUPOA MAFUTA HUCHUJWA

MAWESE YAMEKAMULIWA NA KUCHUJWA VIZURI YAPO TAYALI KWA MATUMIZI YA KUPIKIA

MABAKI YA MAPEKE YA MAWESE HUBANGULIWA NA HUKAMULIWA MAFUTA TENA AMBAYO HUTUMIKA KUTENGENEZA SABUNI.
         KAZI YA KUKAMUA MAFUTA IMEKAMILIKA NASASA TAYALI KWENDA SOKONI

0 comments:

Post a Comment