Pages

Ads 468x60px

Wednesday, February 17, 2016

PANTALEO SHIO DIWANI WA KATA YA MAENDELEO KUMALIZA MGOGOLO SOKOMATOLA


DIWANI WA KATA YA MAENDELEO KUPITIZ CCM PANTALEO SHIO AKIONGEA NA WAFANYA BIASHARA WA SOKOMATOLA
 MFANYA BIASHARA AUSONY MTOKOMA AKIONGEA JAMBO KATIKA MKUTANO HUO
                             JOHN CHUNGWA AKITOA KERO YAKE KATIKA MKUTANO
 MFANYA BIASHARA BEN JOSHUA  MUHANGA WA KUWEKEWA SUPER GLUE KATIKA KUFULI LA MLANGO WAKE AKITOA SHUTUMA KWA MWENYEKITI WA SOKO HILO KUA NDIYE MHUSIKA MKUU WA JAMBO HILO
                                 MKUU WA SOKO OLIVA AMBELE AKIFAFANUA JAMBO
MFANYA BIASHARA JOYCE MWAKASOLE AKITOA KERO YAKE
 MWENYEKITI WA SOKO ABDALLAH SHAIBU AKIKANUSHA TUHUMA ZILIZOJILI JUU YAKE

MWNYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA SOKOMATOLA AKIONGEA JAMBO KATIKA MKUTANO HUO





                     BAADHA YA WAFANYA BIASHARA WALIHUDHULIA MKUTANO HUO

                                                                          HABARI



PANTALEO  SHIO DIWANI WA KATA YA MAENDELEO KUMALIZA MGOGOLO SOKOMATOLA
Akiongea katika na wafanya biashara wa soko hilo kwenye mkutano wa pamoja  wenye lengo la kutaka kujua changamoto zinazo wakabiri wafanya biashara hao Shio amewataka watoa kero zilizopo katika soko hilo ili kuzidafutia ufumbuzi na kuleta amani na utulivu katika soko.

“Mimi kama diwani wenu nimeitisha kutano huu ili kuchukua changamoto na kero zenu ambazo zinawakabiri katika soko hili nimesikia mambo mengi sasa basi kupitia mkutano huu nawataka kila mmoja wenu kusema kila kilichopo katika moyo wake ili tuweze kulitatua na kulimaliza kabisa tatizo lililopo hapa kusudi tufanye biashara kwa amani upendo na utulivu kwakua sisi wote hapa ni ndugu” amesema Shio

Akiongea mmoja wa wafanya biashara hao Ben Joshua amesema katika soko hilo kumekuwepo na mgogoro mkubwa kati yabaadhi ya  wafanya biashara hao na mwenyekiti wa soko hilo Abdallah Shaibu kutokana na itikadi ya vyama jambo ambalo limeleta uhasama mkubwa kati yao na kuligawa pande mbili soko hilo.

Ameongeza kua uhasama huo ambao uliitwa kwa majina tofauti wengine wakisema waunguja na wapemba na wangine wakisema maalshababi umefikia pabaya kufikia kumshutumu kiongozi huyo kutia Super glue katika makufuri ili kushindwa kuyafungua.

Nae John chungwa amesema chanzo cha mgogoro huo ni siku iliyo fanyika usafi kitaifa kwa amri ya Raisi wa jamhuri  ya muungano wa Tanzania John pombe magufuri kuamuru Tarehe 09dec 2015 kwamba badara kuadhimisha sikuku ya uhuru basi siku hiyo itumike kufanya usafi katika maeneo yetu.

Ndipo wafanya biashara wa soko hilo walijiwekea sheria ndogo ya kwamba endapo mtu hata fika ama kuchelewa kufika kufanya usafi basi kutakua na adhabu ya kulipa pesa kiasi cha shilingi elfu mbili kitu ambacha baadhi yao hawakutekeleza sheria hiyo.

Kwa upande wa Mwenyekiti Abdallah Shaibu ambae ndiye aliyetuhumiwa kuanziaha mgogolo huo amekili kuwepo kwa tofauti hizo kati yake na kundi hilo aliloliita alshababi kwamba imetoka na wafanya biashara hao kuto kubaliana na uongozi wake hivyo wamekua wakifanya visa mbalimbali ili kuungusha utawala wake

“Ni kweli mgogoro huo upo ambao umesababisha na kundi la alshababi kutokubaliana na uongozi wangu, Ninao ushahidi wa barua iliyo andikwa na kikundi hiki kwamba hautakuakua tayali kushirikiana na uongozi huu kwa hiyo sioni ajabu kwa tuhuma hizi zi naziendelea zina lengo la kunichafua” amesema Shaibu

Kuhusu tuhuma za yeye kuhusika na utiaji Super glue katika makufuli ya wa baadhi ya maduka ya wafanya biashara hao Shaibu amekanushakua hakuhusika  na kuwataka wanao mtuhumu kuleta ushahidi na kama itadhibitika kua kahusika basi yeye yupo tayali kujiudhuru nafasi hiyo.

                                                                          MWISHO


0 comments:

Post a Comment