Pages

Ads 468x60px

Saturday, February 6, 2016

Wananchi mkoani Mbeya kumeza dawa za Mectizan na Albendazole.



Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amezindua  warsha ya siku moja ya uraghabishi na uhamasishaji juu ya magojwa yaliyokua hayapewi kipaumbele iliyofanyika katika ukumbi wa mkapa jijini hapa

Warsha hiyo iliyo andaliwa na wizara ya afya na maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto kupitia mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokua hayapewi kipau mbele ime jumuisha wadau kama wakuu wa wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, maafisa elimu na madaktali.

Akiongea katika warsha hiyo Kandoro ame wataka viongozi hao kusimamia kwa ukamilifu zoezi la umezeshaji dawa kwa kinga tiba ya magojwa haya ili mkoa wa Mbeya kwa mwaka huu na miaka ijayo iondokane na magonjwa yasiyo pewa kipaumbele.

“Rai yangu kwa Wakuu wa wilaya Wakurugenzi wa Halmashauri na viongozi wa ngazi zote kusimamia kikamilifu zoezi la umezeshaji dawa kinga tiba ya magonjwa haya ili mkoa wetu mwaka huu na miaka ijayo uweze kupata “Coverage” ya umezaji dawa” amesema Kandoro

Ameongeza kua Wakurugenzi wa Halmashauri mpango huu waingize katika mipango yao na kutenga pesa za kutosha za kupambana na magonjwa haya badala ya kutegemea pesa za wahisani tu.

Lakini pia amewaasa Wakurugenzi na maafisa wote wanao husika na mchakato wa kutoa pesa hizi za mradi waache ukilitimba ili pesa hizo zitoke kwa wakati na kuwezesha shughuri hii kufanyika kwa wakati ulio pangwa.

Kwa upande wa wananchi Kandoro amewataka kujitokeza kwa wingi ili kumeza dawa hizo za Kinga tiba kama watakavyo elekezwa na wataalamu wakati wa kampeni husika. Amesema dawa hizi zimethibitishwa na Shirika la Afya nchini kua ni salama na hazina madhara yoyote.

Mkoa wa Mbeya umezeshaji wa dawa hizi za Mectizan na Albendazole kwa kinga tiba ya magojwa ya Matendena mabusha utafanyika tarehe 20 mwezi huu wa Februari na pia utafanyika umezeshaji wa dawa ya Praziquatel na Albendazole kwa ajilia ya kinga tiba ya minyoo pamoja na kichocho kwa  watoto walio na umri wa kwenda shule ugawaji huu utafanyika mashuleni mwezi wa  agosti kwa mwaka huu.
                                   Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akifugua warsha
  Muwezashaji wa warsha Edward Kirumbi Program officar NTD Program wizara ya Afya akileza jambo kuhusiana na matumizi ya dawa.
 
Muwezeshaji wa warsha Dr Boniphace Idindili Envision Program manager akisema neno katika semina hiyo


                                                   Baadhi ya washiriki waliopata nafasi ya kujitmbulisha


                                             Edward Kirumbi muwezesha wa warsha
                  Afisa Elimu mkoa wa Mbeya Charles Mwakalila akichangia mada katika warsha
                                 Mganga mkuu mbarali Dr Boniface Kasululu akichangia mada

0 comments:

Post a Comment