Pages

Ads 468x60px

Monday, September 25, 2017

MWADALLU AWAFUNDA VIONGOZI WA CCM MBEYA.


Katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya mbeya mjini Gerralad Mwadallu amewataka viongozi waliochaguliwa kutoka katika nfasi ya utendaji, Makatibu wa matawi na kata zote wilaya mbeya mjini kua viongozi wenye maadili kwa jamii.

Ameyasema hayo katika Semina ya siku moja kwa viongozi hao iliyo andaliwa na ofisi za CCM wilaya ya mbeya mjini yenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao, semina imefanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Sangu jijini Mbeya.

”Siku ya leo tumeona ni vema kukutana na viongozi wote watendaji ili kuelezana namna ya utendaji ndani ya chama chetu tumewaita watendaji tu ili mjue wajibu katika utekelezaji wa majukumu yenu, Kwakua chama hiki ni kipya hakitaki mtu ambae hayupo tayaki kuwa mchapa kazi kama kuna mtu kaingia kwa bahati mbaya atupishe hatuna utani katika hili” amesema Mwadallu

Ameongeza kua kiongozi anaetakiwa kipindi hiki ni Yule mwenye uelewa juu ya kupambanua mambo,mwenye mwenendo na tabia njema kwa jamii ikiwa ni pamoja na kuwajibika mbele ya umma na kua na kauli nzuri kwa anaowaongoza.

Nae Charles Mwakipesile mjumbe wa kamati ya siasa wilaya ya mbeya mjini alisema wapo watu ambao wamekuwa wakibeza utendaji kazi wa Dk. Magufuli na kwamba kazi hiyo ni sehemu ya Propaganda hivyo Wanaccm wanapaswa kusimama kidete katika kutoa elimu na kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika kipindi kifupi cha uongozi wake.

Aliongeza kuwa wapinzani wamekosa sera za kuwaeleza wafuasi wao badala yake wamejikita katika kuelezea propaganda ambayo lengo lake ni kupotosha na kuelezea uuma na kuaminisha kuhusu uongo jambo linalopelekea kuishia kulalamika kila siku.

Kwa upande wake Katibu wa Wazazi Wilaya ya Mbeya mjini, Sadick Kadulo alisema ili Chama cha Mapinduzi kiendelee kushika dola kwa miaka mingi zaidi lazima kiwe kinafanyiwa mabadiliko na marekebisho ya mara kwa mara ili kuboresha kuendana na wakati.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo waliupongeza uongozi wa CCM Mbeya mjini kwa kuwajali na kuwapa mafunzo na kuongeza kuwa huko nyuma walikuwa wakiongoza kwa kutumia utashi wao na sio kupatiwa semina kama hiyo.

Mwisho.

 VINONGOZI WA KAMATI YA SIASA MBEYA MIJINI NA MJUMBE CHARES MWAKIPESILE AKIONGEA JAMBO KATIKA SEMINA HIYO
KATIBU WA VIJANA WILAYA YA MBEYA MJINI (UVCCM) GERRALD KINAWILO AKIONGEA JAMBO
Katibu wa Wazazi Wilaya ya Mbeya mjini, Sadick Kadulo mmoja wa wakufunzi wa semina hiyo akiongea.








BAADHI YA VIONGOZI WALIOHUDHULIA SEMINA HIYO

0 comments:

Post a Comment