Pages

Ads 468x60px

Tuesday, June 26, 2012


Zaidi ya watuhumiwa (88) wametiwa mbaloni na jeshi la polisi kwa makosa mbalimbali ikiwemo wizi wa kuvunja na kubomoa lakini pia wizi wa mafuta ya magari yanayofanya shughuri za ujenzi wa barabara ya Tunduma na sumbawanga.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda Athumani Diwani amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika msako unaoendelea mkoani mbeya tangu tarehe 08/06/2012 mpaka hivi leo vitu mbalimbali vimekatwa.
Diwani amesema vitu vilivyo kamatwa ni pamoja na pikipiki tatu (3) Zenye usajiri no T489 BQU aina ya Sanya T584 BPU aina ya STAR T301 BRU aina ya saug Vitu vingine ni simu za mkononi,computer laptop, Bunduki mbili aina ya shotgun na Risasi kumi na mbili Vitu vingine ni Tiv, Radio, nk
Kamanda Diwani ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Mbeya kutoa ushirikiano wa kutosha kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za uharifu ili kuliweka mji wetu katika hali ya usalama zaidi, Lakini pia kwa upande wa wa halifu  A mewataka kuacha mara moja kwakua Biashara hiyo haitalipa tena katika mkoa huu.
Kisha akawataka wananchi kufika polisi kituo cha kati kwa ajili ya kuweza kuvitambua vitu vyao iwapo mtu alipotelewa ama kuibiwa kitu.
  Kamanda Athuman Diwani akiongea na Waandishi wa Habari Nje ya ofisi yake mkoani.
 Kamanda Diwani Akionyesha Bunduki mbili zinazozaniwa kuhusika na vitendo vya uharifu zilizo tengenezwa kienyeji na kutumia risasi za kawaida lakini zinauwa.
     Hivi ni Baadhi ya vitu vilivyokamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani mbeya

0 comments:

Post a Comment