Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 17, 2012


Muungano wa jamii  Tanzania (MUJATA) umemuomba radhi  mkuu wa  mkoa wa mbeya Mh.ABBAS KANDOLO kuwa hakupaswa kushutumiwa na wananchi mkoani hapa kuwa alihusika na vurugu za machinga  zilizotokea mwaka jana.
Hayo yamesemwa katika mkutanao uliofanyika  Inyala wilaya ya mbeya vijijini uliowakutanisha  machifu wote wa mkoa wa mbeya, mwanza,shinyanga,Luvuma na Rukwa wenye lengo lakupinga  vikali vitendo  viovu vinavyotendwa na watu wasioutakia mema mkoa wa mbeya.
Wamesema mkuu wa mkoa wa mbeya ABBAS KANDOLO  anastahili kuombwa radhi  kwani wakati wa vurugu za mwanjelwa  alikuwa mgeni katika mkoani hapa  hivyo kumuhusisha na na vurugu ni kumuonea.
Hata hivyo wametaja baadhi  ya vitendo vingi vya uvunjifu wa amani mkoani hapa kuwa ni pamoja na upigaji nondo,kuzika  watu wakiwa hai ,siasa za uchochezi  hali inayosababisha  maandamano na uharibifu  wa rasrimali ukiwemo uchomaji wa barabara.
Mwenyekiti wa machifu mkoa wa mbeya SHAYO SOJA MASOKO amewaomba wananchi mkoani hapa kushiriki  katika ulinzi shirikishi ili kuondokana na vitendo hivyo nakuongeza kuwa vitendo hivyo vinauletea sifa mbaya mkoa huu.
Pia amesema kitendo chakufanya jaribio lakumzika chifu melele ambayo aliokolewa na jeshi la polisi na watu wengine wa wa wili ambao wamezikwa  eneo la itezi uyole na malamba wilayani mbarali  kwa tuhuma zakishirikina.
Amesema matukio hayo yanaendelea kushamili  kutokana na baadhi ya watu baada yakufiwa na ndugu zao wanaenda kwa waganga wa kinyeji  kupiga lamuli ili kujua aliehusika na kifo cha marehemu na hatimaye huambiwa kuwa mtu Fulani  hivyo kusababisha  matendo hayo kuibuka siku hadi siku.
 Kwaupande wake mkuu wa wilaya ya mbeya NOMANY SIGARRA AMBAYE alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa mbeya  amewapongeza viongozi wa ulinzi shirikishi na muungano wa jamii (MUJATA) kwa kuwa mustali wa mbele  kulinda na kupigania haki mkoani hapa.
Amesema serikali  iko tayali  kuunga mkono chama chochote , taasisi ya dini  ama kikindi chochote kinachopigania  amani kwani ni wajibu wa serikali kutetea wananchi wake.
Akizungumzia kuhusu msamaha wa mkuu wa mkoa wa  mbeya  Mh. ABBAS KANDOLO amesema  mkuu huyo ameshasamehe mda mrefu  na hana kinyongo na mtu yeyote Yule kuhusu suala hilo.
Aidha amesema chama chochote ambacho kinapanda jukwaani kutukana matusi kitachukuliwa hatua kali za kisheria kwani kufanya hivyo ni kesi ya jinai nakuongeza kuwa polisi itamushughulikia mwanachama yeyote atakaye jaribu kufanya hivyo.
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nomany Sigarra akisisitiza jambo katika mkutano huo
Mwenyekiti wa machifu Mkoa wa Mbeya Shayo masoko akielezea kitu wakati wa mkutano.
Mwenyekiti wa ulinzi shilikishi Kaijage akikemea vitendo vya uzikzji watu wakiwa hai
 Chifu Matuge akiwa katika pozi la utulivu akiendelea kusikiliza mkutano
 Mkuu wa wilaya ya Mbeya Nomany Sigarra akicheza ngoma za kienyeji zilizokuwa zikitumbuiza katika mkutano.

0 comments:

Post a Comment