Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 17, 2012


Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kimeendelea kuinyama raha CCM baada ya kunyakua viti sita kati ya saba vya uenyekiti wa serikali za mtaa na viti nane kati ya 14 vya wajumbe katika kata mbalimbali zilizoachwa wazi jijini mbeya.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya mbeya mjini JOHN MWAMBIGIJA wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisini za chadema zilizopo manga jijini hapa.
MWAMBIGIJA amesema hii ni ishara tosha ya kukiondoa chama cha mapinduzi  madarakani kwani wao  ni waasisi wakukiondoa chama hicho kikifuatia na vyama vingine ambavyo vipo nchini.
Katika majigambo yake amesema CHADEMA ni Barcelona na CCM ni mtibwa hivyo wataendelea kuangusha kichapo dhidi yao katika  kampeni yao ya twanga kotekote akiliita ni jeshi la NATO hivyo CCM haina pakuchomokea.
Katika uchaguzi huo ambapo wenyeviti ni Richard A mwakalinga mtaa wa benki kata ya Rwanda Willy Chaula mtaa wa karobe kata ya karobe, Ngambi kulagha  mtaa wa ilolo kata ya manga,James mwakalobo mtaa ilemi kata ya ilemi,phillipo mwalukisi mtaa wa tembela Josephat hasara Gunga wa mwanseko.
Na kwaupande wa wajumbe ni Eneya mwansojo mtaa wa ilolo kati ,mtaa wa ilemi Benjamini mbwilo ,Erick Legembo wa mtaa wa mwanseko na wengineo wengi.
Pia amesema  viongozi hao wamechaguliwa ili kuziba nafasi ambazo ziliachwa na watu ikiwemo kuhama vyama  na wengine kupoteza maisha kutoka vyama   mbalimbali jijini hapa.
Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya mbeya mjini John Mwambigija akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chadema.

0 comments:

Post a Comment