Pages

Ads 468x60px

Thursday, August 23, 2012

AUSTRALIA KUONGEZA IDADI YA WAKIMBIZI


Australia imesema itaongeza hadi watu 20,000 kila mwaka idadi ya wakimbizi itakayowapokea nchini humo, ikiwa ni nyongeza ya asilimia 40, na nyongeza kubwa kabisa  tangu kupita miaka 30. 
Hatua hiyo ni mpango wa kuzuia watu kuingia nchini humo kwa magendo. Waziri Mkuu wa Australia, Julia Gillard, amesema mpango huo pia utawapa hifadhi wakimbizi 400  kutokea Indonesia, kama ishara ya nia njema. Awali Australia ilikuwa inachukua wakimbizi 13,750 kwa mwaka.  Australia sasa imesema itashauriana na shirika linalowashughulikia wakimbizi la Umoja wa Mataifa na washirika wake wengine, huku waziri wa uhamiaji, Chris Bowen, akisema wakimbizi wengine watakaohifadhiwa ni wa kutoka Mashariki ya kati, Kusini Mashariki mwa Asia na Afrika. Hatua hii itaifanya Australia kuwa taifa la pili duniani kuwapatia makazi idadi kubwa ya wakimbizi baada ya Marekani.      

0 comments:

Post a Comment