Pages

Ads 468x60px

Monday, June 9, 2014

Serikali imeshauliwa kuwashughulikia wale wote wanao wakashifu waasisi wa Nchi hii



Mzee Isakwisa Mwambulukutu mwenyekiti wa wazee wa chama cha mapinduzi (ccm) akiongea na waandishi wa habari



 wazee wa ccm wakisikiliza kwa makini hotuba ya mwenyekiti kwa waandishi wa habari wakitoa tamko lao

                                             Habari kamili


Serikali imeshauliwa kuwashughulikia wale wote wanao wakashifu waasisi wa Nchi hii.

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa Wazee wa Chama cha mapinduzi mkoani Mbeya Isakwisa Mwambulukutu alipokua akionge katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa Mbeya pic hotel jijini hapa.

Mwambulukutu amesema  hayo alipokua akitoa tamko kwa niaba ya wanachama na wazee wa ccm juu ya kauli mbalimbali zinatolewa katika bunge za kuwakashifu waasisis wa Taifa hili ambao wamekua ndiyo chimbuko la Nchi yetu

“Sisi kama wananchama na wazee wa ccm wa mkoa wa mbeya tunapenda kukemea vikali na kwa nguvu zetu zote na kulaani kauli mbaya zinazotolewa na baadhi ya vijana wetu katika bunge maalum la katiba kwa kuwakafshifu na kuwakejeli waasisi wetu J. k. Nyerere na Amani Karume kwakuwa hao ndiyo chimbuko la Taifa hili” Amesema mwambulukutu

Ameongeza kuwa  kama wanataka kuendelea na Bunge hilo wanapaswa kuwacha mara moja Lugha hizo za kejeli na kashfa  na wajue uhuru wanao utumia unakikomo na  kwamba watanzania wote si wajinga na wanapenda kusikiliza lugha zao wanazotumia.

Pamoja na hayo  wazee  hao wamempongeza Rais na mwenyekiti wa chama hicho J. K Kikwete kwa busara zake na kuruhusu mchakato wa kuunda katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na pia kwa uvumilivu wake katika kuona wanakamilisha jambo hili.

Pia wazee hao  wanaunga mkono mfumo wa Serikali mbili wala si vinginevyo na hawapo tayari kuwasaliti wasisi wa nchi hii isipokua zifanyike juhudi za ziada katika kuondoa kasoro ndogo ndogo zilizopo ndani ya muungano.

0 comments:

Post a Comment