Pages

Ads 468x60px

Thursday, March 26, 2015

Askofu wa kanisa la Moraviani Tanzania jimbo la kusini magharibi Alinikisa Cheyo amewetaka viongozi wa kanisa kuwajibika katika kazi.



Hayo yamebainishwa  leo wakati  akizungumza na mwandishi wa habari hii katika semina ya siku nne iliyoandaliwa na kanisa hilo  inayofanyika katika ofisi za kanisa hilo zilizopo Jakaranda jijini Mbeya.
Askofu Alinikisa Cheyo(picha na maktaba yetu)


Amesema swala la uwajibikaji kwa watendaji wa kanisa  limekua tatizo kubwa ambalo limepelekea kuwepo kwa semina za mara kwa mara kwa wakuu hao ili kuwajengea uwezo katika utendaji  wa kazi zao za kila siku.
                                        
“Watumishi wengi  wamekuwa wakichaguliwa na Halmashauri kuu ya kanisa bila kujua wajibu wao katika kutekeleza majukumu yao mara nyingi hujikuta wanafanya kazi wakisukumwa na roho mtakatifu tofauti na viongozi wanaotoka Serikalini hufanya kazi kwa ufanisi zaidi kuliko hawa” amesema Askofu Cheyo

Nae Zacharia Sichone Makamu mwenyekiti wa kanisa hilo amesema wameamua kuendesha semina hiyo ili kuwajengea uwezo viongozi hao kwa lengo la kuwaimarisha na kuona wanajua wajibu wao ili wakishindwa kutekeleza majukumu yao basi wajihukumu wao wenyewa kukushindwa kutekeleza kinacho wapasa kufanya.

“Tunaweza kulaumiana na kwa makosa mbalimbali kwa wakati mwingine si kwa makosa ya watu kumbe nikutokana na uelewa mdogo walio nao hawajui wajibu wao, Kupitia mafunzo haya kila mmoja atajua kinacho mpasa kufanya na kisha kufikia malengo makubwa na kuleta maendeleo katika kanisa letu” Amesema Sichone.

Kwa upande wake Agripa Senka mkurugenzi wa uchumi, mipango na maendeleo amesema kumekuwepo na mpango wa miaka minne ya kuendesha mafunzo ya namna hiyo  kwa  hivyo kwani viongozi wengi huchaguliwa bila kuwa na maarifa ya uongozi kupitia semina hizo zitafanya viongozi  kuwa na uwezo wa kiutendaji na kujiamini katika kazi zao.

Pia Nyandu Kajange katibu wa wilaya ya chunya ambae ni mmoja wa washiriki wa semina hiyo amesema wamejifunza kusimama vizuri katika nafasi zao nakupanga mipango  ya kazi nyenye utekelezaji mzuri na  kujiamini katika uongozi na kuleta maendelao katika taasisi husika.
                                               mwisho 
 Katibu mkuu wa kanisa la moraviani Tanzania mmoja wa wakufunzi wa semina akiongea jambo wa wanasemina





 Viongozi na wakuu wa taasisi za kanisa la moraviani Tanzania jimbo la kusini magharibi wakisikiliz za kwa makini mafunzo yanayoendelea
          Makamu wa mwenyekiti Zacharia Sichone akijangia moja ya mada katika Semina hiyo
                Devule mwambije mkaguzi wa ndani wa kanisa akongea kitu katika semina

                                                                            Mwisho


0 comments:

Post a Comment