Pages

Ads 468x60px

Monday, March 23, 2015

Mamlaka ya Majitaka na Majisafi ya jijini Mbeya yakili kuwepo kwa tatizo la chemba ya majitaka inayo tililisha maji katika mto wa Dauseni jijini Mbeya kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.



Mamlaka Imeahidi kuijenga chemba hiyo haraka iwezekanavyo ili kuwapunguzia wakazi wa kata ya majengo kero hiyo ndani ya wiki mbili zijazo ili kulinda afya zao dhidi ya magonjwa ya milipuko.

Baada ya kilio cha muda mrefu sasa kwa wakazi wa jiji la Mbeya kata ya majengo kwa kile walichodai kero ya chemba ya majitaka kutililisha maji hayo katika mto wao unaotumika na idadi kubwa ya wakazi hao kwa shughuli mbalimbali za kijamii na kuhatarisha afya zao na kuahidi kuijenga chemba hiyo ndani ya wiki mbili.

Akiongea na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake mkurugenzi mtendji wa mamlaka ya majisafi na majitaka Eng: Simion Shauri amesema hakuwa na taarifa ya tatizo hilo hivyo amewataka wakazi hao kuwa na subira kwani suala hilo litashughulikiwa haraka iwezekanavyo.
 
Eng: Simion Shauri akiongea na wakazi wa majengo,  









“Nawaomba wakazi wa majengo kuwa wavumilivu kwa tatizo walilonalo litatuliwa ndani ya wiki mbili zijazo na kuwafanya waishi kwa amani kama kawaida, ni kweli sikuwa na taarifa ya tatizo hilo la sivyo lingekua tayari limetatuliwa kwa muda muafaka na kuiondoa kero hiyo kwa wakazi ambao wamekua wakilalamika”amesema Shauri.

Ameongeza kutoa wito kwa wakazi wa jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi ili kujiunga na huduma ya mtandao wa uondoshwaji wa majitaka kutoka katika majengo yao na kwa sasa mamlaka imeondoa gharama za kuunganishwa katika mtandao huo na kuwapa mabomba mita 30 bure wateja wake ili kuhamasisha na kuwapa unafuu wa huduma hiyo.
Naye Eng: Mloelya Paul amesema tatizo hilo lilisababishwa na ujenzi wa barabara uliokuwa ukifanywa na Halmashauri ya jiji la Mbeya na kubomoa chemba hiyo na kuziba na hivyo kufanya shughili ya kuizibua kuwa ngumu kwa kua ilizibwa na mawe makubwa ambayo yanatakiwa kuchimbwa ili kuyatoa.
Eng: Mloelya Paul akisoma Risala kwa mgeni rasmi

 “tatizo hilo lipo kwa muda mrefu sasa tulikuwatunashughulikia bajeti yake ambayo mpaka sasa imekamilika ndani ya wiki hii tutaanza kulichughulikia na ndani ya muda wa wiki mbli zijazo litakua limekamilika wakazi hao wategemee kuondokana na kelo hiyo iliyosababishwa ujenzi wa barabara za halmashuri ya jiji ambao hubomoa miuondo mbinu hiyo mwanapoendesha shughuru zao hizo” amesema Mloelya.

Hatua hiyo imekuja baada ya kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa kata ya majengo ambao walikumbwa na mshangao mkubwa baada ya mamlaka hiyo kujenga chemba mpya kwa muda wa masaa 24 na kuizindua katika  maadhimisho ya wiki ya maji na kuicha chembe iliyokua kero kubwa kwao iliyopigiwa kelele kwa muda mrefu na kutopatiwa ufumbuzi,

    Chemba ya majitaka inayotililisha majitaka katika mto Dauseni ambayo ni kero kubwa kwa wakazi wa kata ya majengo

Mto huo maji yake hutumika kwa matumizi mbalimbali kama mwandishi wa habari hii alivyo wakuta wanafunzi wa shule ya Sekondali ya Rejiko wakichota maji hayo yenyekuchanganyikana na majitaka

0 comments:

Post a Comment