Pages

Ads 468x60px

Saturday, March 21, 2015

Sirikisho la vyuo vikuu mkoani Mbeya wamtaka Prof: MARCK MWANDOSYA kujitokeza kuwania uraisi uchaguzi mkuu ujao.


Hayo yamejili katika kongamano la wasomi hao lililohusu uchaguzi  mkuu wa mwaka 2015 na kuonesha nia yao ya kumshawishi kugombea nafasi hiyo.
 IDD MAMBO KATIBU ITIKADI NA UENEZI CHUO KIKUU TEKU AKIMKARIBISHA MSEMAJI WA TAMKO HILO.

 BAADHI YA WANACHAMA WA CCM NA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU WALIOKUWEPO KATIKA KUTOA TAMKO HILO

 OSCAR MWAIHABI KATIBU WA SHIRIKISHO LA WANAZUONI AKITOA TAMKO KWA NIABA YA WANAZUONI MKOANI MBEYA KWA WAANDISHI WA HABARI


Soma hapa:

Na: Charle Abraham


Sirikisho la vyuo vikuu  mkoani Mbeya wamtaka Prof: MARCK MWANDOSYA kujitokeza kuwania uraisi uchaguzi mkuu ujao.

Hayo yamejili katika kongamano la wasomi hao lililohusu uchaguzi  mkuu wa mwaka 2015 na kuonesha nia yao ya kumshawishi kugombea nafasi hiyo

 Katika siku za karibuni kumekuwapo mjadala mkubwa ndani ya CCM juu ya mtu atakayepitishwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho, na ilizidi baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kuwa mwanachama ambaye atateuliwa na CCM kugombea urais hayumo miongoni mwa waliojitokeza na kuwataka wanachama kuwashawishi watu wenye sifa wajitokeze


 Wakati joto la urais likizidi kupanda ndani ya CCM kutokana na hofu ya baadhi ya majina mazito ya wagombea wa nafasi hiyo kuendelea kujitokeza na ikiwa ni pamoja na kujinadi kwa sili hali hiyo imechukua hatua zaidi baada ya shirikisho la vyuo vikuu mkoani Mbeya kufaya kongomano la uchaguzi mkuu  lililofanyika katika ukumbi wa Benjamini Mkapa jijini hapa nakuchukua nafasi hiyo ya kumshawishi Prof: MARCK MWANDOSYA kugombea nafasi ya uraisi.

Akisoma tamko loa wanazuoni hao mbele ya waandishi wa habari katibu wa shirikisho hilo OSCAR MWAIHABI toka chuo kikuu cha tumaini amesema wamefikia uwamuzi huo baada ya kuona ndani ya chama hicho hakuna kiongozi mwenye sifa ya kufanana nae na hivyo wangeona Tanzania ijayo ikiongozwa na kiongozi huyo.

“Sisi wanazuoni tumeona kuwa wewe Prof: MARK  J. MWANDOSYA unafaa kabisa kupokea kijiti cha uraisi kutoka kwa JAKAYA KIKWETE kwakua unafaa ni tofauti na wengine wote waliojitokeza kutangaza nia katika Chama Cha mapinduzi kutokana nauongozi ulio wahi kushiriki kuongoza hujawahi kupata tuhuma yoyote mpaka leo hii, pia Taifa linahitaji kiongozi mwenye hekima na maamuzi magumu hata utafiti unaonesha uwezo ulionao wa kiuongozi” amesema Mwaihabi

Ameongeza kua Mwandosya ni mengi mazuri ameyafanya katika uongozi wake ndani ya Taifa hili, Hivyo wao kama wanazuoni wanamuomba kwa heshima kubwa ashawishike kugombea nafasi hii adhimu katika Taifa hili ya Uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama Cha mapinduzi kama Dr. Jakaya Kikwete alivyo wataka wanachama wa CCM kuwashawishi watu wenye uwezo ambao hawajajitokeza kutangaza nia zao wajitokeze. 

Hadi sasa, wanachama waliojitokeza kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, January Makamba (Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia), Hamisi Kigwangala, na Lazaro Nyalandu ambaye ni waziri wa Maliasili na Utalii.

Lakini pia wako wanaotajwa kuwania urais lakini hawajatangaza ambao ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sita, William Ngeleja, Emmanuel Nchimbi, Mwigulu Nchemba, Stephen Wasira, Bernard Membe na Edward Lowassa ambaye ameibua mjadala kati ya kambi yake na zinazompinga.
                                                                              Mwisho

 

0 comments:

Post a Comment