Pages

Ads 468x60px

Tuesday, March 31, 2015

Sakata la mwanafunzi aliyekutwa amekufa ndani ya shimo la majitaka limechukua sura mpya baada ya wananchi wenye hasira kali kuchukua sheria mkononi baada kuvunja na kuichoma moto nyumba.



Tazama ilivyo anzwa kuchomwa moto
Tatizo la kujichukulia Sheria mkononi limeendelea kuwa kubwa kwa jamii ya watanzania,  katika sakata la hivi karibuni ambapo baadhi ya watu walikuvunja na kuichoma moto nyumba ya mkazi mmoja wa mtaa mbwile b jijini Mbeya kwa tuhuma za kubaka na kumuua mwanafunzi wa miaka nane.
Nyumba ikiwa imebomolewa

Katika hali isiyo ya wakawaida wakazi hao wamejikuta wakichukua sheria mkononi kwa kuivunja na kuichoma moto nyumba ya Mariamu  kasonta baada ya kumtuhumu mlinzi wake kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi majengo mwenye umri wa miaka nane jina limehifadhiwa na kisha kumkuta akiwa ameuwawa na kutupwa katika shimo la maji taka.

Wakazi hao ambao walipimga vibaya mlinzi huyo aliejulikana kwa jina moja la Charles ambae alikamata siku ya tatu tangu kutokea kwa tukio hilo na kuokolewa na askali polisi waliowahi kufika katika eneo la tukio, wananchi hao   walivamia  nyumba ya bosi wake kisha kuibomoa na kuchoma moto ambapo kikosi cha zimamoto kilifika na kufaninikiwa kuuzima moto huo kabla ya kuiteketeza  nyumba hiyo kabisa.






 Askali wa jeshi la polis baada ya kufanikiwa na kuwadhibiti wananchi kiatika kutekeleza uharifu huo
 Mwenyekiti wa mtaa mzee Bukuku akiwataka wakazi wa eneo hilo kuondoka na kuacha kuibomoa nyumba hiyo,
Zunda gabliel kaimu mkuu wa kituo cha polisi  kati akiongea na wananchi kufanya ulinzi wa nyumba iliyokua ikibomolewa
Henry kakobe askali wa kata ya Nonde akiwatuliza wananchi katika mkutano ulioitishwa na mwenyekiti wa mtaa huo.




Wananchi waliofika kwenye mkutano wakitaka  mtu aliehusika na mauwaji ya mwanafunzi atajwe.
Askali kanzu wakiimalisha ulizi katika mkutano wa wananchi wa Nonde Mbeya

Rebeka mwalyego afisa mtendaji wa mtaa wa mbwile (b) akiongea na waandishi wa habari katika eneo la tukio 

0 comments:

Post a Comment