Pages

Ads 468x60px

Saturday, October 14, 2017

WALEMAVU WASHAURIWA KUJIAJIRI KATIKA SEKTA YA BIMA.



ILI kuondokana na tabia ya utegemezi kwa watu wenye ulemavu wa kutokusikia, wametakiwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kujiajiri kwenye uwakala wa bima za vyombo vya moto.

Aidha imeelezwa kuwa kupitia vikundi hivyo wanaweza kuanzisha makampuni ya Uwakala wa Bima na kuweza kuendesha biashara kama watu wengine na hatimaye kujipatia vipato.

Hayo yamesmwa na  Meneja wa Mamlaka ya usimamizi wa  Bima Tanzania (TIRA)  Nyanda za juu kusini,  Consolata Gabone katika  semina ya walemavu  iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha ufundi ( VETA ) jijini Mbeya.

Meneja huyo amesema Watu wenye ulemavu wa kutosikia wanaweza  kujipatia  kipato cha kujikimu kimaisha na kuondokana na uchumi tegemezi kwa jamii inayo wazunguka.

Amesema semina hiyo yenye lengo la kufundisha umuhimu wa Bima kwa jamii ili kuepuka na namna kukabiliana na majanga ya ajali ya vyombo vya moto.

Consolata amesema  mamlaka inao wajibu wa kusajili wadau wa bima, makampuni, mawakala na wakadilishaji wa Hasara ikiwa ni pamoja na kukagua makampuni ya Bima madalali na mawakala pia kushughulikia malalmiko ya bima kutoka kwa wakata bima na jamii kwa ujumla kazi ambayo inaweza kufanywa na mtu yeyote bila kujali hali aliyonayo.
”Nawakaribisha kujiunga katika vikundi ili muweze kuanzisha makampuni na kuja kwetu mamlaka ya usimamizi wa Bima ili tuwasajili na kisha kuanzisha biashara ya uwakala na kujipatia ajira itakayo wapatia kipato kitakacho wakimu katika maisha na kuondokana na utegemezi” Amesema Consolata.

Nae Afisa shirika la bima la ( NIC) jijini hapa, Michael Msata amewataka walemavu hao kuwa na elimu ya bima na  kukata  bima katika shughuli zao mbalimbali ikiwa ni pamoja na bima ya mali, nyumba, ajali, Afya  na nyumba, ili kuepuka hasara endapo kutatokea hasara.

Kwa upande Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye ulemavu wa kutokusikia Mkoa wa Mbeya (CHAVITA) Tusajigwe Mwalwega ameupongeza uongozi huo kwa kutoa semina hiyo kwa makundi maalumu kwani wengi hawajui maana ya bima na kwamba ni kitu cha muhimu katika maisha ya kila mwanadamu.







0 comments:

Post a Comment