Pages

Ads 468x60px

Tuesday, October 31, 2017

WATANZANIA KATIENI BIMA MALI ZENU – DK. SAQWARE.


WATANZANIA wametakiwa kuwa na utaratibu wa Kukatia Bima Mali zao ili kujikinga na hasara pindi majanga mbalimbali yanapotokea na kupelekea vilio kwa Wahanga.

Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Kamishna wa Bima nchini Dk. Baghayo  Saqware alipokuwa akizungumza na mtandao huu kuhusu mwitikio wa Watanzania katika kukata Bima za Mali zao alipokuwa akihani msiba wa Baba mzazi wa Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Bima Nyanda za juu kusini, Elia Kajiba Marehemu Paul Kajiba.

Kamishna huyo alisema kuwa na Bima kunamuondolea hofu ya kupoteza Mali kutokana na kuwa na uhakika wa kuweza kulipwa fidia na Kampuni ya Bima baada ya aidha kupata ajali ya Moto,tetemeko la ardhi au kimbunga kinachoweza kusambaratisha Mali pamoja na mafuriko.

Alitolea mfano Wahanga wa Soko la Sido jijini Mbeya ambao walikumbwa na janga la Moto lililopelekea kuteketeza Mali na bidhaa mbalimbali zilizokuwemo kwenye maduka yao lakini waliokuwa na Bima waliweza kulipwa na hatimaye kupata mitaji ya biashara zao.

Aliongeza kuwa kuna aina nyingi za Bima ambazo kila Mtu anaweza kukata ikiwemo Bima ya Mali, ajali, Maisha na Bima ya Afya kwa ajili ya kuwezesha familia kupata matibabu muda wowote wanapougua.

Hata hivyo akitoa salam za rambi rambi katika ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Moravian Usharika wa Mjini jijini Mbeya na kuzikwa katika makaburi ya Nonde, Kamishna huyo aliwataka jamii kuishi kwa upendo na kufuata matendo mema ya Marehem.

Naye Meneja wa Bima Kanda ya Nyanda za juu kusini, Consolata Gabone alisema upendona mshkamano mahala pa kazi ni ishara ya ushirikiano ambao umeoneshwa na kuguswa na Kamishna hadi kuhudhuria ibada ya mazishi.

“Sio Kawaida kwa Kamishna kuja huku mkoani kushiriki msiba wa kufiwa kwa mfanyakazi wake kwani alikuwa na uwezo wa kutuma mwakilishi hivyo tunajifunza kuishi kwa upendo na mshikamano sehemu zetu za kazi” alisema Gabone.
Meneja wa Bima Kanda ya Nyanda za juu kusini, Consolata Gabone menye brauzi ya kijivu akishiriki ibaada ya mazishi
Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Bima Nyanda za juu kusini, Elia Kajiba mtoto wa marehemu akitoa heshima zake za mwesho


Ndugu, Jamaa na marafiki wakiwa ndani ya ibaada ya mziashi iliyofanyika katika kanisa la Moraviani Mbeya mjini

Msafara wa magari kuelekea makaburi ya Nonde kwa mazishi


Mchungaji wa kanisa la moravia Osia Mbotwa akiongea jambo makaburini
Jeneza lilili chukua mwili wa marehemu Paulo kajiba likishushwa kaburini


0 comments:

Post a Comment